SHIRIKISHO
la Soka Afrika (CAF) limewapa siku 10 Shirikisho la Soka Kongo
(FECOFOOT) kumuwasilisha mchezaji Langa Lesse Bercy mjini Libreville,
Gabon afanyiwe vipimo vya MRI ili kuthibitisha umri wake kama
anaruhusiwa kucheza mashindano ya vijana chini ya umri wa miaka 17.
Katika
kikao cha Kamati ya Utendaji ya CAF jana mjini Libreville, FECOFOOT
wametakiwa kumpeleka mjini humo Langa Lesse Bercy akafanyiwe vipimo
kufuatia malalamiko yaliyowasilishwa na Shirikisho la Soka Tanzania
(TFF), baada ya zoezi hilo kushindikana mara mbili.
TFF ilimlalamikia mchezaji huyo baada ya Kongo kuitoa U-17 ya Tanzania katika hatua ya mwisho ya mchujo wa kuwania tiketi ya fainali za mwaka huu zilizopangwa kufanyika Madagascar.
Awali, Kongo walitakiwa kumpeleka mchezaji huyo makao makuu ya CAF mjini Cairo, Misri kwa vipimo, lakini mara mbili wakashindwa kufanya hivyo.
Wakati huo huo: CAF imeivua uenyeji wa fainali za U-17 AFCON 2017 na imetoa muda hadi Januari 30 mwaka huu nchi nyingine kujitokeza kuomba uenyeji.
Tanzania, walioomba kufanya fainali za 2019 wanaweza kupewa yenyeji wa fainali za mwaka huu iwapo watakuwa tayari.
0 maoni:
Chapisha Maoni