Klabu ya Sunderland imemsaini beki wa zamani wa Aston Villa Joleon Lescott kwa mkataba wa muda mfupi.
Lescott, aliiaga Aston Villa majira ya mwisho baada ya kushiriki msimu mmoja kwa klabu hiyo.
Baadaye alijiunga na AEK Athens, na kushiriki mechi nne na klabu hiyo ya Ugiriki kabla ya kupata jeraha na mkataba wake kufutiliwa mbali mwezi Novemba.
Sunderland iko katika nafasi ya mwisho katika jedwali la ligi ya Premia , wakiwa na alama 15, alama tatu juu timu zilizo hatarini kushushwa daraja.
0 maoni:
Chapisha Maoni