Juuko ni kati ya wachezaji watatu wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara waliopo AFCON, wengine wakiwa na beki wa Yanga Vincent Bossou wa Togo na winga wa Azam, Bruce Kangwa wa Zimbabwe, ambao hata hivyo wenzake wamekwenda mechi mbili bila kucheza.
Juuko alikosa mchezo wa kwanza tu Uganda ikifungwa 1-0 na Ghana, lakini jana alikuwepo uwanjani kwa dakika zote 90, The Cranes ikichapwa 1-0 tena na Misri.
Katika mchezo uliotangulia jana, mshambuliaji Asamoah Gyan aliipeleka Ghana Robo baada ya kufunga bao pekee dakika ya 21 akimalizia krosi ya Jordan Ayew, Black Stars ikiilaza 1-0 Mali.
Michuano hiyo inaendelea leo kwa wenyeji Gabon kumenyana na Cameroon katika mchezo wa Kundi A mjini Libreville ambao wanatakiwa lazima washinde ili kwenda Robo Fainali.
Wakifungwa watatolewa na wakitoa sare itabidi wasikilizie matokeo ya mechi nyingine ya mwisho ya kundi hilo kati ya Burkina Faso na Guinea-Bissau.
Rais wa Gabon, Ali Bongo aliwatembelea wachezaji jana na kipa Didier Ovono akasema: "Rais ametupa hamasa kuelekea mechi hiyo. Hiyo itakuwa fainali yetu ya kwanza."
0 maoni:
Chapisha Maoni