Pages

Jumamosi, 7 Januari 2017

MKWASA KUIDAI TFF FIDIA YA MILIONI 80



Na Alex Mwenda
Aliyekuwa Kocha wa Taifa Stars, Charles Boniface
Mkwasa analidai Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Sh milioni 80 ikiwa ni fedha za malipo ya mshahara wake ambazo hajalipwa kwa miezi kadhaa.


 Image result for mkwasa
TFF imeamua kuachana na Mkwasa hivi karibuni kwa makubaliano kufuatia mkataba wake kutarajia kufikia tamati Machi, mwaka huu kisha kumteua Salum Mayanga kushika nafasi yake hiyo.


Mayanga aliyekuwa akiifundisha Mtibwa Sugar, ana jukumu la kuandaa kikosi kitakachowania kufuzu Kombe la Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (Chan) Aprili mwaka huu.

Mshahara wa Mkwasa kwa mwezi ulikuwa Sh milioni 28 ambao aliurithi kutoka kwa Mart Nooij ambaye alisitishiwa mkataba kutokana na TFF kutoridhishwa na utendaji wake.

Akizungumza, bosi mmoja wa TFF alisema, Mkwasa anadai Sh milioni 80 ambazo anatarajiwa kulipwa kwa mikupuo miwili ndani ya mwezi huu.

“Ni kweli Mkwasa anaidai TFF Sh milioni 80 ambazo zinatokana na malipo ya mshahara wake ambao ulikuwa ukilimbikizwa, hivyo TFF ipo katika hatua za kumlipa fedha zake hizo kabla ya kocha mpya kuanza kazi.

“Fedha hizo zinatarajiwa kulipwa kwa mikupuo miwili 



0 maoni:

Chapisha Maoni