
MEXICO CITY —Maandamano yamezidi kushika kasi nchini mexico baada ya kupandishwa bei ya mafuta kwa asilimia 20 kitu ambacho kimewafanya watu wengi katika miji mbalimbali kuingia mtaani na kupinga ongezeko hilo la bei.
katika maandamano hayo jumamos muandamanaji mmoja aliendesha gari kwa kasi aina ya pickup na kwenda kuwagonga askari waliokuwa wakizuia ghasia katika eneo Baja California.
Msemaji wa jeshi la Polisi amesema hakuna askari alie fariki ila baadhi ya maafisa wamejeruhiwa katka tukio hilo lilitokea karibu na mpaka jiji la Tijuana.
video hii chini inaonesha jinsi gari hiyo pickup ndogo ilivyokuwa ikiendeshwa kwa kasi kuelekea usawa walipo askari na kuwagonga.






0 maoni:
Chapisha Maoni