Pages

Jumapili, 22 Januari 2017

Yahya Jammeh afungasha virago na kutimkia Equatorial Guinea

Aliyekuwa Rais wa muda mrefu wa Gambia, Yahya Jammeh ameondoka nchini humo Jumamosi usiku na kwenda nchini Equatorial Guinea baada ya kushindwa uchaguzi na kugomea kuondoka madarakani hali ambayo ilizifanya nchi za jirani kutumia diplomasia kumuondoa madarakani.



Yaya Jammeh akiwapungia mkono watu alipokuwa akiabiri ndege BanjulJammeh amedaiwa kuondoka na mali za mamilioni ya pesa pamoja na magari ya kifahari.

Mshauri maalumu wa Rais wa Gambia Adama Barrow amesema zaidi ya dola za Kimarekani milioni 11 zinaaminika kutoweka katika hazina ya serikali, kufuatia kuondoka madarakani kwa mtawala wa muda mrefu Yahya Jammeh.

Mia Ahmad Fatty amewaambia Waandishi wa habari katika mji mkuu wa Senegal Dakar kwamba wataalamu wa masuala ya fedha wanatathmini kujua ni kiasi gani kwa sasa kimepotea.

Amesema Gambia kwa sasa ina tatizo kubwa kifedha kwa hazina yake kutokuwa na kitu.

Kwa sasa Rais Barrow amekuwa akifanya kazi na timu ya wataalamu wa masuala ya fedha na wengine kutoka Benki kuu ya nchi hiyo kupata kiasi halisi kilichopo.

Habari zinasema magari ya kifahari na mali nyingine zilionekana zikipakiwa katika ndege ya mizigo ya Chad kwa niaba ya Rais Jammeh siku alipoondoka nchini humo.

Maelfu ya watu walikusanyika katika Ikulu ya nchi hiyo jana jioni wakiyaangalia majeshi ya Senegal yakiingia kwa ajili ya kuweka usalama kabla ya kurejea nchini kwa Adama Barrow.
 Wanajeshi wa Senegal wakishika doria karibu na ikulu ya rais mjini Banjul JumapiliBarrow ambaye aliapishwa Alhamisi kwenye ubalozi wa Gambia nchini Senegal, hivi sasa anatarajiwa            kurejea nyumbani.
alisema atarejea tu baada ya kuhakikishiwa usalama wake.

0 maoni:

Chapisha Maoni