Pages

Jumatano, 4 Januari 2017

Karruache awachana Chris Brown na Soulja Boy

 Image result for CHRIS BROWN BEEF WITH SOULJA BOY
Mwaka 2017 umeanza vibaya kwa Chris Brown na Soulja Boy – kwakuwa wameanzisha bifu chanzo kikiwa ni mrembo Karrueche Tran.
 Image result for SOULJA BOY LIKE KARRUECHE'S PICS
Bifu ya Chris Brown na Soulja Boy inayoendelea imemkera Karruache Tran na ameamua kufunguka. Wasanii hao wameendelea kutupiana vijembe kwenye mitandao ya kijamii baada ya kuingia ugomvi ambao Karruache aliyekuwa mpenzi wa Breezy anahusishwa.

 Image result for CHRIS BROWN BEEF WITH SOULJA BOY
Tangu alipoachana na Karrueche Chris amekuwa akimfuatilia mrembo huyo huku mara kadhaa akigombana na wanaume ambao wanaomtolea udenda. Na sasa balaa limemkumba rapper Soulja Boy baada ya kulike picha ya mrembo huyo kwenye mtandao wa Instagram kitendo ambacho kimeonekana kumkera Brown.

Mrembo huyo ameiita drama ya wasanii hao kuwa ni ya kijinga na haina maana yoyote hata katika mwaka mpya. Amewaomba wamtoe kwenye malumbano yao.

Tazama alichokiandika pamoja na jibu la Chris Brown..
Untitled
karucheeeHii inshu yote ilikuja baada ya Soulja Boy kufunguka kupitia mtandao wa Twitter kuwa Chris amemtafuta na kumpiga mikwara baada ya kulike picha hiyo.



Chris Brown amekuwa akijaribu mara kadhaa kutaka kurudiana na Karrueche lakini imekuwa ngumu kwa mrembo huyo kukubali.

0 maoni:

Chapisha Maoni