Pages

Jumanne, 7 Februari 2017

Okwi aanza mechi ya kwanza Villa kwa sare

Na Alex Mwenda
Mshambuliaji wa zamani wa klabu za Yanga na Simba, Emmanuel Okwi leo ameanza rasmi kuitumikia klabu yake ya SC Villa Jogoo kwa kuichezea mechi ya kwanza dhidi ya Bright Stars.
Okwi alianza mechi hio ya Ligi Kuu nchini Uganda iliyomalizika kwa sare ya bila kufungana na kuwaacha Villa wakiwa nyuma ya vinara KCCA kwa pointi tatu.
 Image result

Awali Okwi aliuambia mtandao huu kuwa yupo fiti kucheza mchezo wa leo lakini hafahamu kama kocha atamuanzisha.

Wageni Villa walitawala mchezo huo kwa kiasi kikubwa lakini Okwi na wenzake walishindwa kabisa kuisumbua safu ya ulinzi ya Bright Stars.
Okwi amejiunga na Villa kwa mkataba wa miezi sita akitokea klabu ya Denmark aliyoamua kuachana nayo baada ya kukosa namba katika kikosi cha kwanza kwa muda mrefu.

0 maoni:

Chapisha Maoni